Wajinga watatawala, mikoa tusipoamka,
Naitoa halahala, uchaguzi tunataka,
Ila pasiwe na hila, kiongozi kumuweka,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Ukiritimba watula, vigumu kuneemeka,
Uchama sasa ni hila, mikoa inavunika,
Na wajuu watawala, kile kisichostahika,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Shamba la bibi walola, viongozi wastahika,
Kila mmoja apula, kile anachokitaka,
Si mashamba si mihela, wazidi kutakasika,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Usimwamshe alolala, hilo wanalitamka,
Hawana kwako jamala, ila wao kulimbika,
Na hili kila pahala, hija sasa yafanzika,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Madaraka kijumla, lazima kujayashika,
Mikoa kujitawala, kiuchumi kwa hakika,
Rasilimali ni ghala, ziache kuja ibika,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Na huu si ukabila, kiongozi twamtaka,
Mkoa mwenye jamala, waziri mkuu kumweka,
Na mawaziri salala, wizarazo kuzishika,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Na hili sio suala, wakubwa rai kutaka,
Ni ukoloni wa msala, kuacha hawatayataka,
Wazidi kuwa madhila wadhani wanajengeka,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Watu acheni kulala, mikoa kutawalika,
Ubwege nao ufala, bado hamjauchoka,
Mikoa sio jalala, wabovu kujawaweka,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
Tusiendelee kulala, mikoa ije jengeka,
Ujerumani kulola, haya yanavyofanyika,
Ni raha yangu Makilla, mikoa kuongozeka,
Mikoa tusipoamka, kuzidi kudidimia.
DIWANI YA MASHAIRI
Saturday, November 5, 2011
Udaktari si hoja
Kuna digrii za bandia, nyingine za kupewa,
Dukani huko India, si vigumu kununua,
Kisomo lebo haijawa,bali uwezo nao kuwa,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Wengi tunaowajua, udakta wajivunia,
Ndani ukiangalia, hawana wanalojua,
Kitu wangelitambua, masikini tusingekuwa,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Ni sponchi zilojaa, maji huya kumwaia,
Pulizo zilopepewa, upepo ndani kujaa,
Abyadhi kifungua, akili zimetopea,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Udokta bwana kujua, kila unachoangalia,
Na unayojisemea, kuhakiki unajua,
Na kila unachosikia, tathmini kukifanzia,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Hesabu huzitambua, japo hutozielewa,
Kujumlisha sanaa, na kuzidisha hatua,
Ni mtu wa kutambua, mfuko sio gunia,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Si wa kuwaitikia, wachimvi wanaolia,
Wanasiasa kugwaya, kufanza wanayoamua,
Japo ujinga wajua, bado unawatumikia,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Sio kashfa nazua, watu budi kujijua,
Nafasi kutochukua, mahala pasipowafaa,
Na ushaur kujitia, hali huna unalojua,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Huruma ninawaonea, dokta jina kupewa,
Wengi wachangamkia, hata tiba asilia,
Marais waingia, ni nyingi wajizolea,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Mawaziri nao pia, sasa wanajipatia,
Wengine wazinunua, nafasi kujiongezea,
Mbumbumbu walokuwa, sasa ni maprofesaa,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Ila anzali ajua, hujui hujayajua,
Na kilemba si kofia, na wigi sio upaa,
Kibla wanaojua, uongo hawatazua,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Dukani huko India, si vigumu kununua,
Kisomo lebo haijawa,bali uwezo nao kuwa,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Wengi tunaowajua, udakta wajivunia,
Ndani ukiangalia, hawana wanalojua,
Kitu wangelitambua, masikini tusingekuwa,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Ni sponchi zilojaa, maji huya kumwaia,
Pulizo zilopepewa, upepo ndani kujaa,
Abyadhi kifungua, akili zimetopea,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Udokta bwana kujua, kila unachoangalia,
Na unayojisemea, kuhakiki unajua,
Na kila unachosikia, tathmini kukifanzia,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Hesabu huzitambua, japo hutozielewa,
Kujumlisha sanaa, na kuzidisha hatua,
Ni mtu wa kutambua, mfuko sio gunia,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Si wa kuwaitikia, wachimvi wanaolia,
Wanasiasa kugwaya, kufanza wanayoamua,
Japo ujinga wajua, bado unawatumikia,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Sio kashfa nazua, watu budi kujijua,
Nafasi kutochukua, mahala pasipowafaa,
Na ushaur kujitia, hali huna unalojua,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Huruma ninawaonea, dokta jina kupewa,
Wengi wachangamkia, hata tiba asilia,
Marais waingia, ni nyingi wajizolea,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Mawaziri nao pia, sasa wanajipatia,
Wengine wazinunua, nafasi kujiongezea,
Mbumbumbu walokuwa, sasa ni maprofesaa,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Ila anzali ajua, hujui hujayajua,
Na kilemba si kofia, na wigi sio upaa,
Kibla wanaojua, uongo hawatazua,
Udaktari si hoja, hoja umesoma wapi?
Vita viogopeni
Chanzo wasioamua, yapaswayo amuliwa,
Kwa wakati unaofaa, na haki kutengenea,
Siasa wanaotumia, visingizio kadhaa,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Waoga wa kuamua, shujaa wa kuongea,
Ujanja wanaotumia, mahala pasipofaa,
Na za mkato njia, watakaozitumia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Kadiri wasiojua, yatakiwa kugawiwa,
Ukiritimba kuzua, fikra unapoua,
Na mabavu kutumia, dhidi ya wao raia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Haambiliki balaa, hakuna wanalosikia,
Kaburi hujichimbia, huku wanajionea,
Na hutaka kuingia, na wale wanowafatia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Uwezo wasiokuwa, ila wingi wa tamaa,
Ukubwa wanaolilia, hata watu kuwaua,
Nafsi wasiojua, tayari kuangamia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Uchama wanaotumia, uhalali kujitia,
Wananchi kuwagawa, majinuni wasojua,
Na kisha kuwatumia, malengo yao kufikia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ni watu walolaniwa, toka walipozaliwa,
Na Mola huwasaidia, motoni kuja ingia,
Na laiti walingejua,ukubwa wangeukataa,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Mamlaka wasoachia,pale wanapotakiwa,
Wakatafuta wabaya,kumbe wao ndo wabaya,
Bahaluli kutumia, mauti kuyaandaa,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Katiba wakiwambiwa, si wao kuiandaa,
Ulaghai wajitia, na kughushi washtakiwa,
Wawaacha wanasheria,wajifanya wanajua,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ufisadi waulea, na mafisadi radhia,
Kwa mali wakiwafaa, chamani na nyumbani pia,
Na aibu wala haya, vigumu kujionea,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ni watu wasosikia, sikio linalojifia,
Ushauri huambaa, mradi wakajifanyia,
Kilio kinachofatia, hakitawasumbua,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ni muda kujiandaa, vijana wa Tanzania,
Nchi wanaochezea, lazima kuwafichua,
Kizazi kinachofatia, amani kikailea,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Kwa wakati unaofaa, na haki kutengenea,
Siasa wanaotumia, visingizio kadhaa,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Waoga wa kuamua, shujaa wa kuongea,
Ujanja wanaotumia, mahala pasipofaa,
Na za mkato njia, watakaozitumia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Kadiri wasiojua, yatakiwa kugawiwa,
Ukiritimba kuzua, fikra unapoua,
Na mabavu kutumia, dhidi ya wao raia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Haambiliki balaa, hakuna wanalosikia,
Kaburi hujichimbia, huku wanajionea,
Na hutaka kuingia, na wale wanowafatia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Uwezo wasiokuwa, ila wingi wa tamaa,
Ukubwa wanaolilia, hata watu kuwaua,
Nafsi wasiojua, tayari kuangamia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Uchama wanaotumia, uhalali kujitia,
Wananchi kuwagawa, majinuni wasojua,
Na kisha kuwatumia, malengo yao kufikia,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ni watu walolaniwa, toka walipozaliwa,
Na Mola huwasaidia, motoni kuja ingia,
Na laiti walingejua,ukubwa wangeukataa,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Mamlaka wasoachia,pale wanapotakiwa,
Wakatafuta wabaya,kumbe wao ndo wabaya,
Bahaluli kutumia, mauti kuyaandaa,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Katiba wakiwambiwa, si wao kuiandaa,
Ulaghai wajitia, na kughushi washtakiwa,
Wawaacha wanasheria,wajifanya wanajua,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ufisadi waulea, na mafisadi radhia,
Kwa mali wakiwafaa, chamani na nyumbani pia,
Na aibu wala haya, vigumu kujionea,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ni watu wasosikia, sikio linalojifia,
Ushauri huambaa, mradi wakajifanyia,
Kilio kinachofatia, hakitawasumbua,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Ni muda kujiandaa, vijana wa Tanzania,
Nchi wanaochezea, lazima kuwafichua,
Kizazi kinachofatia, amani kikailea,
'Siombe vita vibaya, chanzo wasioamua!
Thursday, October 20, 2011
Uhuru wa kiuchumi
Uchumi kuwa huria, twataka viranja wapya,
Fani wanaozingatia, na ustadi kujaliwa,
Wajifanyao wajua, hatutaki wasikia,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Nchi hii ni dunia, mipaka imesambaa,
Tunatakiwa mikoa, yote kujitegemea,
Huru ikaachiwa, uchumi kuunyanyua,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Asiwe wa kuteua, mkuu wetu wa mkoa,
Twataka kumchagua, kiongozi anayefaa,
Uchumi kuuinua, mkoa wetu ukapaa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Awajibike jamaa, kwa wakazi wa mkoa,
Kama inavyoendelea, Ujerumani Ulaya,
Nchi imejigawa, huru mikoa ikawa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Uwekezaji wakua, viwanda vyashindaniwa,
Uzalishaji wakua, na masoko yazagaa,
Hadi sasa wasaidia, homa waliozidiwa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Magari washadidia, BMW mwazijua,
Mercedes Benz radhia, ndiko zinakotokea,
HIi mali ya mkoa, kwa nchi inachangia,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Kilimo wamekomaa, walima kiteknolojia,
KIla mkoa wazaa, cha kula na kujiuzia,
Mayuro wajivunia, na nchi inaendelea,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Biashara waingia, kimataifa wapaa,
China wanakouzia, vyombo vyaaminiwa,
Mjerumani kifaa, nani asiyemjua,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Ni mikoa kutumia, soko, viwanda kua,
Raia kugombania, wao vya kwao bora kua,
Ni heshima na ushujaa, zikiwa bora bidhaa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Elimu wanaojua, watoto kutufundushia,
Mitaala kuchagua, nchi inayoiifaa,
Na masomo kupungua, si ya kikapu kujaa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Huduma wlaiobobea, wafaa wao kutoa,
Pasiwe wa kulegea, kazi akakabidhiwa,
Nchi kuendelea, imara tunatakiwa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Wazee watasogea, pembeni wakasinzia,
KIla wakishtuliwa, mambo wataangalia,
Nchi itasisimua, na wengine kuvutia,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Vijana kuangalia, wapi tuanelekea,
Nasi bila kubagua, nafasi kuwamwagia,
Na wale wanaojua, kutufikisha hatua,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Hakuna kupendelea, hata kwa tuliowazaa,
Kama wasipojua, vingine kuwasaidia,
Ila kama wanajua, wastahili kwendelea,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Fani wanaozingatia, na ustadi kujaliwa,
Wajifanyao wajua, hatutaki wasikia,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Nchi hii ni dunia, mipaka imesambaa,
Tunatakiwa mikoa, yote kujitegemea,
Huru ikaachiwa, uchumi kuunyanyua,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Asiwe wa kuteua, mkuu wetu wa mkoa,
Twataka kumchagua, kiongozi anayefaa,
Uchumi kuuinua, mkoa wetu ukapaa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Awajibike jamaa, kwa wakazi wa mkoa,
Kama inavyoendelea, Ujerumani Ulaya,
Nchi imejigawa, huru mikoa ikawa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Uwekezaji wakua, viwanda vyashindaniwa,
Uzalishaji wakua, na masoko yazagaa,
Hadi sasa wasaidia, homa waliozidiwa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Magari washadidia, BMW mwazijua,
Mercedes Benz radhia, ndiko zinakotokea,
HIi mali ya mkoa, kwa nchi inachangia,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Kilimo wamekomaa, walima kiteknolojia,
KIla mkoa wazaa, cha kula na kujiuzia,
Mayuro wajivunia, na nchi inaendelea,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Biashara waingia, kimataifa wapaa,
China wanakouzia, vyombo vyaaminiwa,
Mjerumani kifaa, nani asiyemjua,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Ni mikoa kutumia, soko, viwanda kua,
Raia kugombania, wao vya kwao bora kua,
Ni heshima na ushujaa, zikiwa bora bidhaa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Elimu wanaojua, watoto kutufundushia,
Mitaala kuchagua, nchi inayoiifaa,
Na masomo kupungua, si ya kikapu kujaa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Huduma wlaiobobea, wafaa wao kutoa,
Pasiwe wa kulegea, kazi akakabidhiwa,
Nchi kuendelea, imara tunatakiwa,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Wazee watasogea, pembeni wakasinzia,
KIla wakishtuliwa, mambo wataangalia,
Nchi itasisimua, na wengine kuvutia,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Vijana kuangalia, wapi tuanelekea,
Nasi bila kubagua, nafasi kuwamwagia,
Na wale wanaojua, kutufikisha hatua,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Hakuna kupendelea, hata kwa tuliowazaa,
Kama wasipojua, vingine kuwasaidia,
Ila kama wanajua, wastahili kwendelea,
Uhuru wa kiuchumi, wataka vinara wapya!
Mapinduzi ya uchumi
Yote tisa sasa kumi, uchumi kuzungumzia,
Sio wewe sio mimi,hapa ndipo pakuanzia,
Nchi bila ya uchumi, siasa hazitafaa,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Mapinduzi ya uchumi, budi kuzungumzia,
Ni vipi tunajihami, utandawazi waingia,
Kuendelea si ngumi, ila uchumi kuzaa,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Kuizindua jamii, majukumu kuyajua,
Miundombinu na lami, barabara kupaua,
Tufanane na Miami, Marekani ilivyokua,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Mbona watu hatutumi, meli kujitengezea,
Treni nazo uchumi, twazitaka kunyanyua,
Na kwanini hatusemi, bandari kujijengea,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Iwe ni wewe na mimi, akili tunatumia,
Ufundi wetu rasmi, kazini ukaingia,
Kusaidiwa uvumi, Magharibi kwasinyaa,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Elimu yetu uchumi, yastahili sasa kua,
Matatizo kujihami, na fursa kuzitumia,
Ni wewe na mimi, twapaswa vitu kuvumbua,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Kwanini hatuwatumi, wana Uchina kujua,
Na njia hatuzifumi, kujifunza Malaysia,
Maslahi si salami, waijuayo Ulaya,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Kwanini hatujipimi, tuone tunapopwaya,
Nchi yataka ulimi, mapya unayozua,
Kisiasa kujihami, watu haijawasaidia,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Sio wewe sio mimi,hapa ndipo pakuanzia,
Nchi bila ya uchumi, siasa hazitafaa,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Mapinduzi ya uchumi, budi kuzungumzia,
Ni vipi tunajihami, utandawazi waingia,
Kuendelea si ngumi, ila uchumi kuzaa,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Kuizindua jamii, majukumu kuyajua,
Miundombinu na lami, barabara kupaua,
Tufanane na Miami, Marekani ilivyokua,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Mbona watu hatutumi, meli kujitengezea,
Treni nazo uchumi, twazitaka kunyanyua,
Na kwanini hatusemi, bandari kujijengea,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Iwe ni wewe na mimi, akili tunatumia,
Ufundi wetu rasmi, kazini ukaingia,
Kusaidiwa uvumi, Magharibi kwasinyaa,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Elimu yetu uchumi, yastahili sasa kua,
Matatizo kujihami, na fursa kuzitumia,
Ni wewe na mimi, twapaswa vitu kuvumbua,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Kwanini hatuwatumi, wana Uchina kujua,
Na njia hatuzifumi, kujifunza Malaysia,
Maslahi si salami, waijuayo Ulaya,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Kwanini hatujipimi, tuone tunapopwaya,
Nchi yataka ulimi, mapya unayozua,
Kisiasa kujihami, watu haijawasaidia,
Tuzungumzie pia, mapinduzi ya uchumi.
Ndoa na chama kimoja
KAMA mnavyotambua, upacha yetu tabia,
Mme na mke twajua, ni wawii kijinsia,
Na kushoto na kulia, ni pande mbili za njia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Wabunge wanapojaa, bungeni kwenda kukaa,
Wote wa chama ikawa, basi jua hapo jaa,
Rahisi kurubuniwa, patupu ukaambulia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
'Ndio' wataitikia, hata kama ni kukuua,
Ili mradi wapewa, posho zenye manufaa,
Haliyo hawatoijua, wala kuizingatia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Vijijini mwaumia, chama mosi kuwaoa,
Vichwa vimewajaa, wenyeviti wasojua,
Kijiji kinadumaa, ni vigumu kuendelea,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Wanasiasa balaa, sikuzote huwahadaa,
Watoto huwadhania, hamtawashtukia,
Pipi mtazingojea, mwaishia kuzisikia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Vyema ndoa kukataa, waume wawili wakawa,
Mkeo kimoja ikiwa, wewe cha pili kuingia,
Yanga na Simba kuwa, wallahi mtaendelea,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Kama nyote Yanga mwawa, nyumba itasinzia,
Au simba tu mkawa, huzubaa familia,
Msisimko hujaa, vyama vingi kuingia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Chagua kuendelea, ukiritmba kataa,
Chama kimoja balaa, hakiwezi kukutetea,
Wao wenyewe hung'aa,wewe ukawa wafubaa,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Ushindani maridhia, ndivyo unavyotakiwa,
Pande mbili kuvutia, kule mtu alikokaa,
Na nchi inaposogea, hatuwapi wasiofaa,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Mme na mke twajua, ni wawii kijinsia,
Na kushoto na kulia, ni pande mbili za njia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Wabunge wanapojaa, bungeni kwenda kukaa,
Wote wa chama ikawa, basi jua hapo jaa,
Rahisi kurubuniwa, patupu ukaambulia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
'Ndio' wataitikia, hata kama ni kukuua,
Ili mradi wapewa, posho zenye manufaa,
Haliyo hawatoijua, wala kuizingatia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Vijijini mwaumia, chama mosi kuwaoa,
Vichwa vimewajaa, wenyeviti wasojua,
Kijiji kinadumaa, ni vigumu kuendelea,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Wanasiasa balaa, sikuzote huwahadaa,
Watoto huwadhania, hamtawashtukia,
Pipi mtazingojea, mwaishia kuzisikia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Vyema ndoa kukataa, waume wawili wakawa,
Mkeo kimoja ikiwa, wewe cha pili kuingia,
Yanga na Simba kuwa, wallahi mtaendelea,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Kama nyote Yanga mwawa, nyumba itasinzia,
Au simba tu mkawa, huzubaa familia,
Msisimko hujaa, vyama vingi kuingia,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Chagua kuendelea, ukiritmba kataa,
Chama kimoja balaa, hakiwezi kukutetea,
Wao wenyewe hung'aa,wewe ukawa wafubaa,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Ushindani maridhia, ndivyo unavyotakiwa,
Pande mbili kuvutia, kule mtu alikokaa,
Na nchi inaposogea, hatuwapi wasiofaa,
Ndoa na chama kimoja, hukufikisha pabaya.
Ukiritimba
Udikteta ndoto mbaya, mjinga akija kuwa,
Akiongoza huumia,wajinga na wanaojua,
Ni watu wa kupepewa, na moto kukokewa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Na huyu mtu akiwa, mwenyewe tu huamua,
Zimbabwe angalia, sasa kinachotokea,
Na Malawi kaingia, mtu tusiyemdhania,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Gaddafy haukujua, yaliyomfika Libya?
Mubarak anajuria, Misri aliyoyazua,
Na Kenya hukuijua, Moi alipsimamia?
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Museveni naye pia, haya hatukumdhania,
Uganda kaikomboa, na sasa anaibomoa,
UKubwa una hatia, kwa watu wasiosikia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Muumba namshangaa, watu hawa kuvumilia,
Sijui anadhania, watakaa kujutia,
Akawapa msamaha, mauti hajawajia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Hujifanya wanajua, hata wasiyoyajua,
Wengine huwadhania, mabaya kuwafanzia,
Kwao si kazi kuua, ukubwa kuutetea,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Shirika nalo balaa, dikteta huliua,
Ukititimba huzaa, maradhi yasiyotibiwa,
Hadi huja kusinyaa, lenyewe likajifia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
TTCL angalia, ugonjwa hatujajua,
Ukimwi utadhania, wala hautaelewa,
Mbona wengine wang'aa, lenyewe lazidi fubaa?
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
TANESCO ni baa, giza na bei kupaa,
Hakuna asiyejutia, 'ovataimu' kuliua,
Wingi wa watu kujaa, na kazi zinazubaa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
TRC ng'amua, na TAZARA inayosinyaa,
Ukiritimba waviua, ushindani unapwaya,
Mameneja wenye njaa, ni shamba la kujivunia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Ukiritimba tabia, wananchi isyofaa,
Na hii ya chama ikiwa, wanachama huenguliwa,
Mamluki wakajaa, mifuko yao kujaa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Na ujinga nahofia, hili unalisaidia,
Wafuasi wakijua, uongozi hupindua,
Udhaifu kukataa, na wengine kuchagua,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Chama kibaka kikiwa, nchi kuisanzulia,
Wananchi huwa wakiwa, wasijue pakukimbilia,
Nusura haitatokea, bila sauti kutoa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Ni sauti ya kukataa, kwa hapo tulipofikia,
Mapinduzi kuyazua, watu wapya kwingia,
Afueni kuitwaa, nchi ipate endelea,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Akiongoza huumia,wajinga na wanaojua,
Ni watu wa kupepewa, na moto kukokewa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Na huyu mtu akiwa, mwenyewe tu huamua,
Zimbabwe angalia, sasa kinachotokea,
Na Malawi kaingia, mtu tusiyemdhania,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Gaddafy haukujua, yaliyomfika Libya?
Mubarak anajuria, Misri aliyoyazua,
Na Kenya hukuijua, Moi alipsimamia?
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Museveni naye pia, haya hatukumdhania,
Uganda kaikomboa, na sasa anaibomoa,
UKubwa una hatia, kwa watu wasiosikia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Muumba namshangaa, watu hawa kuvumilia,
Sijui anadhania, watakaa kujutia,
Akawapa msamaha, mauti hajawajia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Hujifanya wanajua, hata wasiyoyajua,
Wengine huwadhania, mabaya kuwafanzia,
Kwao si kazi kuua, ukubwa kuutetea,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Shirika nalo balaa, dikteta huliua,
Ukititimba huzaa, maradhi yasiyotibiwa,
Hadi huja kusinyaa, lenyewe likajifia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
TTCL angalia, ugonjwa hatujajua,
Ukimwi utadhania, wala hautaelewa,
Mbona wengine wang'aa, lenyewe lazidi fubaa?
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
TANESCO ni baa, giza na bei kupaa,
Hakuna asiyejutia, 'ovataimu' kuliua,
Wingi wa watu kujaa, na kazi zinazubaa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
TRC ng'amua, na TAZARA inayosinyaa,
Ukiritimba waviua, ushindani unapwaya,
Mameneja wenye njaa, ni shamba la kujivunia,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Ukiritimba tabia, wananchi isyofaa,
Na hii ya chama ikiwa, wanachama huenguliwa,
Mamluki wakajaa, mifuko yao kujaa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Na ujinga nahofia, hili unalisaidia,
Wafuasi wakijua, uongozi hupindua,
Udhaifu kukataa, na wengine kuchagua,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Chama kibaka kikiwa, nchi kuisanzulia,
Wananchi huwa wakiwa, wasijue pakukimbilia,
Nusura haitatokea, bila sauti kutoa,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Ni sauti ya kukataa, kwa hapo tulipofikia,
Mapinduzi kuyazua, watu wapya kwingia,
Afueni kuitwaa, nchi ipate endelea,
Ukiritimba mbaya, huongozwa na wajinga!
Subscribe to:
Posts (Atom)