Sikuomba, umenipa, silipi wala sisepi!
Hili huwezi kukwepa, ni jembamba kama papi,
Usiulete mshipa,hujui tuko wangapi?
Silipi wala sisepi, umenipa sikuomba!
Wengi walienda kapa, uliza ni mara ngapi?
Na kwenyewe hapa hapa, na wala hatuongopi,
Huwezi hesabu chupa, ukajalipwa kwa chupi,
Silipi wala sisepi, umenipa sikuomba!
Je, unaye golikipa, na wafungaji wangapi,
Ushindi huwezi kopa, ukope benki ipi?
Utoacho umetupa, silipi wala sisepi,
Silipi wala sisepi, umenipa sikuomba!
Nyenzo yako bado bapa, ukaionolee wapi?
Kenya shilingi ni chapa, kwetu madafu na pipi,
Fisi ukimshinda mfupa, watakaoula wa wapi?
Silipi wala sisepi, umenipa sikuomba!
Moshi wavaa malapa, huku Buguruni vipi?
Mtoto sasa ni pampa, zimeshafubaa nepi,
Ninunualo hulipa, la kupewa sililipi,
Silipi wala sisepi, umenipa sikuomba!
Sijahusudu Urapa, ya kwetu asili iwapi?
Ya wengine ukikopa, ribaye maisha mafupi,
No comments:
Post a Comment